Ticker

6/recent/ticker-posts

Team Kiba kukubali Kichapo cha 4-2 dhidi ya Team Samatta

Team Kiba kukubali Kichapo cha 4-2 dhidi ya Team Samatta


Kikosi cha TeamKiba kimekubali kichapo cha mabao 4-2 dhidi ya TeamSamatta katika mchezo maalum wa kuchangia fedha kwa ajili ya vifaa vya kujifunzia wanafunzi uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi hiyo ilianza kwa kasi ambapo TeamKiba walianza na kasi kubwa mshambuliaji Ibrahim Ajibu alitikisha nyavu mara mbili ndani ya kipindi cha kwanza.

Mohammed Samatta aliipatia TeamSamatta alisawazishia  bao la kwanza na kuweza kufanya dakika 45 za kwanza kumalizika kwa TeamKiba ikiwa mbele kwa mabao 2-1.

Kipindi cha pili kilianza kwa TeamSamatta kuja juu zaidi ikilishambulia lango la TeamKiba na kuweza kujipatia mabao matatu kupitia kwa Haruna Moshi 'Boban', Jamhuri Julio na Mbwana Samatta.

Mpaka dakika 90 zinamalizika, TeamSamatta ilikuwa 4, TeamKiba 2.


____________________________________________________________________ ASANTE KWA KUFUNGUA POST HII Tuna kusihii endelea kutembelea blog yetu ili upate kujifunza meng pia kwa kupakua nyimbo mpya kila Siku ********************************************************* Je? Wewe ni msanii au mfanya biashara Je? Wahitaji tangazo au mziki wako uwafikie watu weng Tangaza mziki biashar tangazo NK. hapa wasiliana nasi 0757136484 Email. Kingsevenmedia@gmail.com

Chapisha Maoni

0 Maoni