B |
Staa maarufu kutokea Colombia Shakiraambaye alitamba na ngoma zake kali zikiwemo nyimbo kama ‘Wakawaka’, Hips don’t lie , Whenever na nyingine nyingi ambazo zilimpatia umaarufu mkubwa duniani.
Katika mahojiano aliyoyafanya naSunday Mirroralikiambia chombo hicho kuwa alikuwa na ndoto kubwa za kuwa mwanamuziki mkubwa alivyokuwa mdogo lakini ndoto hizo zilikuwa zikijaribu kuzimwa na mwalimu wa kwaya shuleni kwao na kumwambia kuwa hawezi kuimba bali anaimba kama mbuzi.
Maneno hayo yalimuumiza sana lakini pia yalimpa nguvu na kufanya mazoezi zaidi katika uimbaji wake hadi kutimiza ndoto yake na kufikia kupata tuzo mbalimbali kama MTV music award Best choreography 2006, Wimbo bora wa mwaka katika tuzo za Grammy 2016 , Best Female artist MTV Europe Music Award 2005 na nyingine nyingi.
Kwa sasa Shakira ameolewa na mchezaji mpira Gerard Piqueanayechezea timu ya Barcelona na wamefanikiwa kupata watoto wawili.
____________________________________________________________________ ASANTE KWA KUFUNGUA POST HII Tuna kusihii endelea kutembelea blog yetu ili upate kujifunza meng pia kwa kupakua nyimbo mpya kila Siku ********************************************************* Je? Wewe ni msanii au mfanya biashara Je? Wahitaji tangazo au mziki wako uwafikie watu weng Tangaza mziki biashar tangazo NK. hapa wasiliana nasi 0757136484 Email. Kingsevenmedia@gmail.com
0 Maoni
King seven tz